We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, March 24, 2019

TANZIA: Mchezaji wa Kagera Sugar afariki dunia


Kiungo wa Kagera Sugar, Behewa Sembwana amefariki dunia leo alfajiri kutokana na kuugua tumbo. 

Kiungo huyo amesumbuliwa na maumivu ya tumbo kwa muda mrefu, hali ambayo ilimlazimu kufanyiwa operesheni takribani mara mbili. 

Nahodha wa timu hiyo, George Kavila amethibitisha kuwa Behewa amefariki baada ya kusumbuliwa na maumivu ya tumbo ambayo alianza kulalamika tangu wakiwa pamoja kikosini. 

“Nakumbuka alianza kuumwa wakati tunacheza na Mwadui, alishindwa kutoka na sisi kwenda kule Complex baada ya hapo alipelekwa hospitali alipatiwa matibabu, lakini baadaye alihamishiwa Muhimbili ndio mauti yakamkuta akiwa hapo,” alisema Kavila. 

Aliongeza kwamba mchezaji huyo ameondoka akiwa na umri mdogo licha na alikuwa amebarikiwa kipaji hasa katika kuuchezea mpira anapokuwa yupo uwanjani.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list