We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, March 28, 2019

Serikali mkoani Kagera yatenga zaidi ya mil. 20 kwaajili ya Vijana

Serikali Mkoani Kagera imetenga zaidi ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya Vijana waendesha pikipiki maarufu kama (BODABODA) ili waweze kujiendeleza katika shughuli za ujasiliamali, na kuacha kutegemea shughuli moja.
Hayo yamesemwa mkoa Kagera na mkuu wa mkoa huo, Brigedia Jenerali Marco Erisha Gaguti alipokuwa akizungumza waendesha pikipiki, wakati wa uzinduzi wa mashindano ya mpira wa miguu yajulikanayo kama JPM BODABODA CUP 2019, ambapo amewataka vijana hao kutumia fursa hiyo muhimu ili kuweza kujiinua kiuchumi.
“Vijana wana dhima na jukumu kubwa la kulinda amani ya nchi yetu kupitia shughuli wanazozifanya kikubwa ikiwa ni matumizi bora ya Vyombo vya Moto, Vijana wataelimishwa zaidi masuala ya Usalama barabarani, namna ya kujiepusha na uhalifu pamoja na elimu ya ujasiliamali,”amesema Gaguti
Aidha, ameongeza kuwa kupitia mashindano hayo serikali inaimani kubwa kwamba upo uwezekano wa kupungua kwa majanga ya uhalifu kwasababu vijana hao watakuwa wamepewa elimu ya kuweza kuwatambua wahalifu na kusaidia kutoa taarifa na ushirikiano kwa jeshi la polisi pamoja na kupunguza ajali za barabarani.
Kwa upande wake mwenyekiti wa usalama barabarani mkoa wa Kagera, Euston Kabantega amewataka vijana hao kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wenzao waendesha bodaboda kwa kuhakikisha wanafuata na kutii sheria zote za usalama barabarani ili kuhakikisha wanakuwa salama wao pamoja na abiria wao wakati wa safari.
Mashindano ya JPM BODABODA CUP 2019 Kagera, yanayoratibiwa na Ofisi ya Mkuu Wa Mkoa Kagera kwa Kushirikiana na Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama barabarani yataanza kutimua vumbi rasmi Jumamosi ya Tarehe 30, Machi mwaka huu kwa kuzishirikisha Timu 16 za Waendesha Bodaboda Manispaa ya Bukoba, huku zawadi zikitajwa kuwa ni pamoja na Kombe kwa Washindi Tatu Bora, pamoja na pesa Sh. Milioni 6 ambapo mshindi wa kwanza atajipatia kitita cha shilingi millioni 3, mshindi wa pili shilingi millioni 2 na mshindi wa tatu shilingi millioni 1

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list