We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, March 26, 2019

Rais Magufuli akwara tuzo ya heshima ya ukuzaji kiswahili Afrika

Chama cha Wanafunzi wa Kiswahili wa Vyuo Vikuu vya Tanzania (CHAWAKITA) kimetoa Tuzo ya Heshima kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Magufuli kutokana na mchango wake mkubwa wa kuthamini na kukuza lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Tanzania.
Image result for rais magufuli tuzo
Rais Magufuli
Tuzo hiyo, imetolewa na chama hicho na kupokewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza kwa niaba ya Rais Magufuli.
Alipokea tuzo hiyo juzi mjini Morogoro wakati akifunga kongamano la 11 la kitaifa la Chawakita lililofanyika Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro.
Kongamano hilo la siku nne lilibeba kaulimbiu inayosema, “Kiswahili, Hazina ya Afrika kwa Maendeleo Endelevu” na kuandaliwa kwa tuzo kwa washindi wa uandishi wa vitabu vya hadithi fupi pamoja na ya heshima ambayo aliyotunukiwa Rais Magufuli kutokana na anavyoenzi na kukitilia maanani Kiswahili.
Pia tuzo nyingine ya heshima ilitolewa kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutokana na mchango mkubwa wa wizara hiyo katika kusimamia na kuendeleza lugha ya Kiswahili nchini.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list