Mlinda lango namba moja wa Simba na Stars Aishi Manula, huenda akahitaji siku kadhaa za mapumziko baada ya kupata majeraha wakati akiitumikia Taifa Stars kwenye mchezo dhidi ya Uganda juzi
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema Manula hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kilichofanya maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya Mbao Fc Jumapili
Wakati huo huo Aussems amesema wachezaji wote wa Simba waliokuwa na majukumu ya timu za Taifa wanatarajiwa kuanza kuwasili leo kuungana na wenzao ambao walianza mazoezi juzi kwa ajili ya maandalizi ya michezo inayofuata
Ukiondoa Aishi Manula, wachezaji wengine wanaotarajiwa kuripoti kambini kuanzia leo ni John Bocco, Jonas Mkude, Erasto Nyoni, Emmanuel Okwi, Juuko Murshid, Meddie Kagere na Clatous Chama
No comments:
Post a Comment