We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, March 4, 2019

Magogo ya kukatia Nyama marufuku nchini


Na. Mussa Enock Dodoma

Bodi ya nyama Tanzania, inatarajia kuanzisha Operesheni nchi nzima ya kukamata na kuchoma magogo yanayotumika kukatia nyama kwenye mabucha ikisema kuwa kufanya hivyo kutasaidia watumiaji wa kitoweo hicho, kula nyama ambayo haina uchafu wowote.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama, Imani Sichalwe kwenye Mkutano Mkuu wa shirikisho la wanachama wa biashara ya mifugo na nyama Tanzania (TALIMETA), uliofanyaka Jijini Dodoma ambapo akijibu hoja ya Mwenyekiti wa wauza nyama Jijini Arusha Alex Lasiki kuhusu upatikanaji wa mashine za kukatia nyama nchini.

Akijibu hoja hiyo, Sichalwe amesema wafanyabiashara hao wanatakiwa kuyaondoa magogo hayo mara moja na kutumia mashine za kukatia nyama na kwamba mashine hizo zinapatikana nchini kwa gharama nafuu.

Akizungumzia juu ya wafanyabiashara wanaouza nyama kwenye ndoo Sichalwe amesema kufanya hivyo ni kinyume cha sheria, huku akitumia nafasi hiyo kuwataka wenye tabia hiyo kuacha mara moja.

Kwa upande wake Afisa nyama wa Bodi hiyo Edgar Mambo, amesema nyama ikikatwa kwenye Gogo na kuhifadhiwa kwenye Friji baada ya muda hubadilika rangi kutokana na uchafu unaokuwepo kwenye gogo hilo.

Katibu mkuu wa TALIMETA, Raphael Chacha amebainisha baadhi ya changamoto zinazowakabili ikiwa ni pamoja na usimamizi hafifu wa machinjio nchini unaoruhusu uuzaji holela wa nyama na kupelekea wao kupata hasara na kufilisika.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list