We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Saturday, March 23, 2019

BANKA YAMKUTA TENA YANGA, ATUPWA NJE

Issa Mohamed ‘Mo Banka’.
KIUNGO mchezeshaji wa Yanga, Issa Mohamed ‘Mo Banka’ yamemkuta tena kwenye timu hiyo baada ya enka yake kuvimba kwenye mguu wake wa kushoto.
Banka amepata majeraha hayo ikiwa ni siku chache tangu arejee kuichezea timu hiyo kwenye kikosi cha Mkongomani, Mwinyi Zahera baada ya kutoka kifungoni.

Kiungo huyo, alikutana na adhabu ya kufungiwa mwaka mmoja na Fifa baada ya kukatana na skendo ya kutumia madawa wakiwa kwenye michuano ya Chalenji iliyofanyika nchini Kenya akiwa anaichezea timu ya Taifa ya Zanzibar Heroes.

Akizungumza na Championi Jumamosi, mratibu wa timu hiyo, Hafidh Saleh alisema kuwa kiungo huyo amepewa mapumziko maalum huku akiendelea na matibabu baada ya enka yake kuvimba.

Saleh alisema, kiungo huyo ameondolewa kwenye mipango ya kocha msaidizi wa timu hiyo Mzambia, Noel Mwandila kwa ajili ya kumtumia katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Alliance United utakaopigwa Machi 30, mwaka huu.

“Banka ameondolewa katika mipango yetu ya mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho kutokana na uvimbe mkubwa uliokuwepo katika enka aliyoipata akiwa mazoezini.

“Tofauti na Banka, mchezaji mwingine atakayeukosa mchezo ni Mwinyi, Abdul wote wana malaria, Dante maumivu ya misuli na Ninja anayetumikia kifungo cha michezo mitatu,” alisema Saleh.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list