We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, February 24, 2019

Rais wa Korea Kaskazini Atumia Treni kwenda Vietnam kukutana na Rais Trump

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un yumo ndani ya treni akielekea nchini Vietnam kwa ajili ya mkutano wake wa pili wa kilele na rais Donald Trump wa Marekani. 

Kim ameambatana na Kim Yong Chol, ambaye ndie mpatanishi muhimu katika mazungumzo na Marekani. Mkutano wa pili baina ya Kim na Trump umepangwa kufanyika Jumatano na Alhamis wiki ijayo mjini Hanoi. 

Mkutano wa kwanza uliofanyika nchini Singapore mwezi Juni, ulimalizika bila ya makubaliano muhimu juu ya kusistishwa miradi ya kinyukilia ya Korea Kaskazini. 

Katika mkutano huo, wataalamu wanasema Kim atajaribu kuimarisha mahusiano na Marekani pamoja pia na kuondolewa vikwazo. Safari za nje za kiongozi huyo wa Korea Kaskazini kawaida hupangwa kwa siri. 

Zaidi ya siku mbili zitahitajika kwa treni anayosafria Kim kuzunguka masafa ya maelfu ya kilomita kupitia mji wa mpakani wa China-Dandong hadi Vietnam.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list