We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, February 25, 2019

Ndoo 226 zenye sampuli za miamba ya madini 883 Zakamatwa Jijini Mwanza

Kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Mwanza inalishikilia gari lori aina Fuso lililokuwa likisafirisha shehena ya sampuli za madini kutoka mkoani Geita kwenda jijini humo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella jana alisema gari hilo lilikamatwa jana na ndoo 226 zenye sampuli za miamba ya madini 883 mali ya Mgodi wa Dhahabu Geita (GGM).

“Gari hilo lilikamatwa na askari waliokuwa doria baada ya kubaini wahusika walikuwa na upungufu wa vibali vinavyoruhusu kusafirisha mzigo huo kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine,” alisema.

Mongella alisema shehena hiyo ilikuwa ikisafirishwa kwenda kwenye maabara ya kupima madini hayo ya SGS iliyopo jijini Mwanza.

Kutokana na hali hiyo, mkuu huyo wa mkoa aliagiza kuchunguzwa na kufuatilia uhalali wa sampuli hizo huku akiwataka watendaji wa Serikali kufanya kazi kwa uadilifu.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list