Uongozi wa Yanga unaandaa mkakati wa ushindi dhidi ya Zesco mabosi wa timu hiyo wakijipanga kufanya kile walichofanya Botswana kwenye mchezo dhidi ya Township Rollers
Baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Zesco katika mchezo uliopigwa Dar, Yanga inahitaji kushinda mchezo wa marudiano utakaopigwa siku 10 zijazo nchini Zambia
Tayari Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshindo Msolla amesema timu hiyo itakwenda kuweka kambi Zambia ili kuhakikisha wachezaji wanazoea mazingira jambo ambalo pia litawasaidia kupunguza presha ya mchezo
Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Hamad Islam amewataka Watanzania na mashabiki wa Yanga wasikatishwe tamaa na matokeo yaliyopita na badala yake wazidi kushikamana mpaka mwisho.
Isalam amesema lengo lao ni kuhakikisha timu inakwenda kufanya vizuri ugenini na kurudi na matokeo mazuri nyumbani na suala la kuitupa nje Zesco United linawezekana kama walivyoifanyia Township Rollers mjini Gaborone.

No comments:
Post a Comment