We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, September 11, 2019

Viongozi wanaotoa ahadi hewa, waandaliwa mkakati


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Damas Ndumbaro amesema serikali imekuwa ikifanya vikao vya majadiliano kuhusu viongozi mbalimbali wanaokuja nchini  kutoka nje na kutoa ahadi bila kuzitekeleza ili kufikia muafaka.

Dk. Ndumbaro ameyasema hayo, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Tauhida Cassian, maelezo ya serikali juu ya viongozi hao wanaokuja nchini.

“Je, serikali ina maelezo gani juu ya viongozi wanaokuja Tanzania na kutembelea baadhi ya maeneo na kisha wanapokuta miradi ya wananchi huahidi kusaidia na baadaye kushindwa kutimiza ahadi zao,” amehoji mbunge.

Akijibu swali hilo, Dk. Ndumbaro amesema ahadi ambazo hutolewa na baadaye kushindwa kutimizwa wizara huratibu vikao vya majadiliano vinavyoshirikisha wahusika pamoja na wizara za kisekta na taasisi za kiserikali ili kupata muafaka juu ya suala husika.

“Tanzania imekuwa ikipokea viongozi wageni kutoa nje ya nchi katika makundi mawili, yaani viongozi hao hutembelea kwa safari za kiserikali na binafsi ambapo hupata fursa ya kuona miradi ya wananchi.

“Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikaino wa Afrika Mashariki, ina jukumu la kuratibu na kusimamia safari za kikazi kutoka mataifa ya kigeni ikiwa ni pamoja na kufuatilia utekelezaji wa ahadi mbalimbali zinazotolewa na viongozi hao kwa kushirikiana na wizara za kisekta na taasisi kiserikali,” amesema.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list