We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Sunday, September 15, 2019

Tetesi za usajili barani ulaya Leo Jumapili

Mchezaji nyota wa zamani wa England, David Beckham ameongezea nguvu mipango yake ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi.

messiHaki miliki ya pichaAFP

Beckham anamiliki klabu ya soka nchini Marekani ijulikanayo kama Inter Miami, ambayo imeshatuma wawakilishi wake kuzungumza na baba wa Messi. (Sun on Sunday)
Inter Miami pia wanataka kumsajili winga wa Real Madrid na timu ya taifa ya Wales, Gareth Bale, 30.(Maxifoot - in French)

kroosHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Manchester United wanapanga kumsajili kiungo Mjerumani wa klabu ya Real Madrid Toni Kroos, 29, mwezi Januari katika mkataba wa kubadilishana wachezaji.
United wanaweza wakamtoa Paul Pogba na kukubali kiasi cha pesa kama sehemu ya makubaliano hayo. (Bild - in German)

pogbaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Kipa wa Uhispania David de Gea, 28, ametia saini mkataba mpya wa miaka minne na Man United wa thamani ya pauni 250,000 kwa wiki, na malipo yanaweza kupanda mpaka pauni 350,000 kwa wiki kulingana na kiwango cha mchezo. (Sunday Mirror)
Mshambuliaji wa England Callum Hudson-Odoi, 18, anatarajiwa kuingia makubaliano mapya na klabu yake ya Chelsea mara baada ya kupona majeraha yake. (Sun on Sunday)
Liverpool wameanza mazungumzo ya kuongeza mkataba na mshambuliaji wake raia wa Senegali Sadio Mane. (SoccerLink, via Sport Witness)

erickHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Kiungo wa Denmark Christian Eriksen, 27, anasubiria uwezekano wa kuihama klabu ya Tottenham na kuelekea Real Madrid, mwezi Januari. (Marca - in Spanish)
AC Milan na Inter Milan wote wana mipango ya kumsajili kiungo Mserbia Nemanja Matic, 31, kutoka Manchester United mwezi Januari. (Corriere Dello Sport - in Italian)
Manchester United wametuma wachunguzi wake kumuangalia mshambuliaji wa Fenerbahce ya Uturuki Vedat Muriqi, 25, wakati akiichezea timu yake ya taifa ya Kosovo dhidi ya England wiki iliyopita. (Sunday Express)

steve

Kocha wa Newcastle Steve Bruce amepewa ridhaa na uongozi wa klabu ya kusajili wachezaji wapya mwezi January, hususani mawinga. (Chronicle)
Mshambuliaji wa Juventus na Croatia Mario Mandzukic, 33, ambaye alikuwa akihusishwa na kutaka kuhamia Man United hivi karibuni, anakaribia kukamilisha usajili wa kuelekea Marekani katika klabu ya LAFC. (Calciomercato)
Beki raia wa England Tyrone Mings, 26,amesema alishangazwa sana pale Aston Villa walipoamua kumsajili kwa pauni milioni 20 kutoka klabu ya Bournemouth. (Express and Star)

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list