We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, September 10, 2019

Prezzo afuata nyayo za Jaguar, Professor Jay na Sugu, Ajitupa rasmi kwenye siasa

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Kenya, Jackson Makini almaarufu kwa jina la Prezzo ametangaza rasmi kuingia kwenye siasa kwa kuchaguliwa nafasi ya kugombea ubunge katika jimbo la Kibra nchini humo.
Prezzo ameteuliwa na Chama cha Wiper leo Jumanne Septemba 10, 2019,  mbele ya kiongozi wa Chama hicho,  Kalonzo Musyoka ambaye alishawahi kuwa makamu wa Rais wa Taifa hilo.
Taarifa hiyo imepokewa na kwa mikono miwili na Wakenya, Huku wengi wakimlinganisha na msanii mwenzie wa muziki, Jaguar ambaye yeye kwasasa ni Mbunge wa Jimbo la Starehe.
Kalonzo anaamini kuwa kutokana na ukumbwa wa Prezzo,  Anauwezo mkubwa wa kuchukua jimbo hilo kwenye uchaguzi utakaofanyika Novemba 7 mwaka huu.
Prezzo atapambana na mwakilishi mwingine wa Chama cha ODM, Imran Okoth kwenye kinyang’anyiro cha kusaka ubunge kwenye jimbo hilo la Kibra.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list