Familia ya rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe imekubali kiongozi huyo azikwe kwenye makaburi ya mashujaa wa kitaifa mjini Harare.

Hata hivyo, tarehe rasmi ya kuzikwa kwake bado haijawekwa wazi. Msemaji wa familia ya Mugabe Leo Mugabe amewaambia waandishi habari kwamba machifu wa kikabila katika eneo alikozaliwa Mugabe ndiyo waliofikia uamuzi huo.
Leo ambaye ni mpwa wa Mugabe amesema mazishi hayo yatakuwa ya kifamilia na wanaendelea kujadiliana kuhusu siku atakayozikwa kiongozi huyo wa zamani. Mugabe alifariki dunia wiki iliyopita nchini Singapore akiwa na miaka 95.

Familia yake na rais Emmerson Mnangagwa, aliyekuwa mshirika wa Mugabe walijikuta wakivutana kuhusu wapi atakapozikwa Mugabe baada ya mwili wake kuwasili nchini humo.
No comments:
Post a Comment