We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, September 18, 2019

Ligi ya mabingwa Ulaya kuendelea leo

Mshike mshike wa ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu wa 2019/20 utaendelea tena leo usiku kwa michezo ya makundi manne kuchezwa katika viwanja tofauti.
Michuano hiyo inayoleta msisimko karibu duniani kote, imerejea kwa kishindo baada ya mashabiki kuanza kushuhudia vumbi likitimka usiku wa kuamkia leo kwa michezo ya makundi manne kuchezwa.
Kwa mshtuko mkubwa mabingwa watetezi Liverpool walianza vibaya kwa kufungwa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya SSC Napoli, huku mabingwa wa soka nchini Hispania FC Barcelona wakilazimisha sare ya bila kufungana dhidi ya Borussia Dortmund.
Timu ya mtanzania Mbwana Samatta KRC Genk nayo ilianza vibaya michuano hiyo kwa kufungwa mabao sita kwa mawili, huku nahodha na mshambuliaji huyo wa Taifa Stars akifunga moja ya mabao ya kufutia machozi.
Leo itakua zamu ya makundi A,B,C na D, baada ya kushuhudia michezo ya makundi E,F,G na H ikichezwa usiku wa jana.
Kundi A
Club Brugge Vs Galatasaray
Paris Saint-Germain Vs Real Madrid
Kundi B
Olympiacos Vs Tottenham Hotspur
FC Bayern Munich Vs FK Crvena Zvezda
Kundi C
Dinamo Zagreb Vs Atalanta
Shakhtar Donetsk Vs Manchester City
Kundi D
Atletico Madrid Vs Juventus
Bayer Leverkusen Vs Lokomotiv Moscow

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list