We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Tuesday, September 10, 2019

Kinachoendelea kesi ya kuua na kumchoma moto mke

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, leo Septemba 10 ilikuwa inaendelea kusikiliza kesi ya mauaji inayomkabili mfanyabiashara Khamis Saidy, anayekabiliwa na mashtaka ya kumuua na kisha  kumchoma moto Mke wake.

Akizungumza Mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Salum Ally, Wakili wa Serikali Wankyo Simon amesema kuwa, upelelezi wa kesi hiyo upo katika hatua za mwisho ili kuipatia mahakama hiyo nyaraka na hatimae kesi hiyo kupelekwa Mahakama Kuu.
Kufuatia maelezo hayo, mshtakiwa aliomba kupatiwa hati ya mashtaka yanayomkabili ambapo wakili Wankyo, aliahidi kumpatia na kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 24, itakapofikishwa mahakamani hapo tena kwa ajili ya kutajwa.
Mfanyabiashara huyo anakabiliwa na mashtaka ya kuua kwa kukusudia, ambapo inaelezwa alitekeleza kosa hilo Mei 15, 2019, mara baada ya kumuua kisha kumchoma na moto wa magunia mawili ya mkaa mke wake Naomi Marijani, kisha kuyachukua mabaki ya mwili huo na kwenda kuyafukia shambani kwake Mkuranga.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list