We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, September 16, 2019

Azam waogope hiki kutoka kwa Triangle United

Kocha wa klabu ya Triangle United, Taurai Mangwilo ametaja kitu kimoja kikubwa ambacho anajivunia katika klabu yake na kitakachowasaidia kusonga mbele kwenye mchezo wa marudiano.


Katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho uliofanyika Jumapili, Septemba 15 Jijini Dar es Salaam, Azam FC imepoteza kwa bao 1-0, huku bao hilo pekee la Triangle likifungwa na Ralph Kawondera katika dakika ya 34.
Akizungumza baada ya mchezo huo, kocha wa Triangle amesema kuwa kitu pekee wanachojivunia ni rekodi yao ya kutopoteza mchezo wowote ambao wanakuwa wa kwanza kupata bao.
"Sisi kama timu hatujawahi kupoteza mchezo wowote ambao tumetangulia kupata bao, kwahiyo matarajio yalikuwepo kwenye mchezo ule. Tulijaribu kuwasukuma ili tupate bao na tulipolipata tukajiamini kuwa tayari tuna kitu kikubwa sana", amesema Mangwilo.
Azam FC inatarajia kusafiri hadi nchini Zimbabwe kwenye mchezo wa marudiano dhidi ya Triangle, ambapo inahitaji kushinda ugenini kwa idadi ya mabao mawili au zaidi ili iweze kusonga mbele katika hatua ya makundi ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list