Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems ameeleza kufurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa leo uwanja wa Uhuru na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1
Akizungumza baada ya mchezo huo, Aussems amesema timu ilicheza vizuri na wangeweza kuibuka na ushindi mnono zaidi kama wangetumia nafasi nyingi walizotengeneza
Mbelgiji huyo amesema atafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza hasa kwenye umaliziaji
"Tumecheza mchezo mzuri dhidi ya timu nzuri. Tumemiliki mpira na kutengeneza nafasi ambazo zimewezesha kufunga magoli mawili tu lakini tulikuwa na nafasi ya kufunga magoli mengi zaidi. Tutafanyia kazi zaidi hilo ili kutumia vizuri nafasi nyingi ambazo tunazipata," amesema

No comments:
Post a Comment