Uongozi wa klabu ya Simba umepanga muda wa mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa dhidi ya UD Songo
Mchezo huo utapigwa Jumapili August 25 saa 10 jioni
Msemaji wa Simba Haji Manara amewataka mashabiki kuendeleza utamaduni wa kuiunga mkono timu yao kwenye michuano hiyo kwa kujaza uwanja siku ya Jumapili
"Kwetu mashabiki sio mchezaji wa 12, ni mchezaji wa kila nafasi uwanjani. Tunashinda lakini mashabiki wanachangia sana," Manara aliwaambia waandishi wa habari kwenye Mkutano uliofanyika Serena Hotel
"Simba ndio timu ambayo imeongoza msimu uliopita kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kujaza mashabiki uwanjani. Tunataka tuliendeleze hilo mwaka huu"
"Na bahati nzuri mchezo wetu wa Ligi ya Mabingwa umepangwa siku nzuri. Utakuwa Jumapili saa 10 jioni"
"Tunataka mashabiki mshabikie mwanzo mwisho, tusisubiri mpaka Shiboub apige mtu chenga, mashabiki tunaenda uwanjani kushabikia"
"Kwa mashabiki wa Simba hii ni Champions League, kazi yetu mashabiki ni kushabikia, twendeni"
"Matumaini yangu tutawatoa UD Songo. Kwa maandalizi yetu, mipango na mapenzi ya Mungu tutashinda"
"Tunawategemea mashabiki waje kutujazia uwanja, waje kutushangilia. Nawaomba Wanasimba tuje kwa wingi kuhakikisha tunaenda kujaza uwanja na tunashinda."

No comments:
Post a Comment