We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Wednesday, August 21, 2019

Man United yaomba msaada kwa kampuni za mitandao

Klabu ya Manchester United imeeleza kusikitishwa na kauli za kibaguzi za mashabiki wa klabu hiyo zinazoelekzwa kwa kiungo wake Paul Pogba kufuatia kukosa penalti katika mchezo wa ligi dhidi ya Wolves.

Katika mchezo huo, Pogba alikosa penalti katika dakika ya 68 ya mchezo, ambapo mwisho wa mchezo timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.
Sehemu ya taarifa iliyotolewa na Manchester United kuhusu suala hilo imesema, "kila mmoja hapa Mmanchester United amesikitishwa na ubaguzi unaoendelea juu ya Paul Pogba kwa kilichotokea usiku wa jana, tunlaani kwa nguvu kitendo hicho".
"Yoyote anayefanya kitendo hiki hawakilishi thamani na ukubwa wa klabu yetu na inatia faraja kuona mashabiki wakilaani suala hili katika mitandao ya kijamii. Tunafanyia kazi kuwafahamu wachache waliohusika katika suala hilo na kuwachukulia hatua kali. Pia tunahimiza makampuni ya mitandao ya kijamii kuchukua hatua kwenye hili", imeendelea kusema taarifa hilo.
Man United ina alama nne mpaka sasa katika michezo miwili iliyocheza, ikishinda mchezo wa kwanza dhidi ya Chelsea na kutoka sare mchezo wa pili dhidi ya Wolves, Jumatatu Agosti 19.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list