We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, June 6, 2019

Namungo FC wazidi kuchafua hali ya hewa

Msimu timu mbalimbali zinaendelea kujiandaa na usajili kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania bara, Namungo FC imeendelea kutikisa katika usajili.

Namungo FC yenye makao yake makuu wilayani Ruangwa mkoani Lindi imeendelea kutikisa katika usajili, ambapo hadi sasa imesajili wachezaji wanne watakaoitumikia timu hiyo msimu ujao.
Mchezaji wa kwanza ambaye imemsajili ni Bigirimana Blaize kutoka Alliance FC, ambapo amesaini mkataba wa mwaka mmoja. Mwingine ni Daniel Joram ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo. Joram aliitumikia Namungo FC kwa mkopo msimu uliopita akitokea Mbeya City.
Pia Namungo FC imeimarisha mikataba ya wachezaji wake wawili, mlinzi, Jukumu Kibanda pamoja na mshambuliaji Lusajo Reliants kwa mkataba wa miaka miwili. 
Kutokana na usajili wanaoufanya Namungo FC, kuna kila dalili ya timu hiyo kufanya vizuri msimu ujao kama ilivyokuwa kwa klabu ya KMC katika msimu wake wa kwanza uliomalizika, ambapo imemaliza nafasi ya nne ya msimamo na kufuzu kucheza michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list