Msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara amemuomba Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Paul Makonda kuifikiria klabu ya Simba kuipatia ardhi kama alivyofanya kwa Yanga na TFF
Akizungumza leo kwenye Harambee ya kuichangia Taifa Stars, Manara amesema Simba itakuwa kama imetengwa kama juhudi zote walizofanya msimu uliopita hazitatambuliwa
"Umewapa watani zetu ekari saba, leo TFF umewapa ekari 15, basi nasisi tunaomba utufikirie," amesema
"Mafanikio yote tuliyopata kwa kufika robo fainali ligi ya mabingwa msimu uliopita!, tulipambana lakini tunashangaa mbona hututaji katika neema hizi za ardhi?"
"Nakuomba sana Mkuu wangu, naamini hatuwezi kukosa ekari mbili..tatu nasi tujidai"

No comments:
Post a Comment