We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, May 30, 2019

Fedha za vitambulisho vya JPM zawatokea puani

Katibu Tawala Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, Tusubilege Benjamin ameagiza jeshi la polisi kuwashikilia watendaji 15 wa vijiji na kata kwa tuhuma za kutafuna fedha zaidi ya milioni 15 za vitambulisho vya wajasiriamali.
Akitoa agizo hilo, Katibu Tawala amesema kuwa kati ya watendaji 29 wa wilaya hiyo, ni watendaji 12 pekee wamesalimika kwenye mkasa huo huku mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Ericki Minga akisisitiza hatua kali za kisheria kuchukuliwa kwa watendaji hao ambao wameitia doa halmashauri.
Aidha, inaelezwa kuwa watendaji hao wamekula pesa za vitambulisho zaidi ya 762 vya wajasiliamali vilivyotolewa na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Halima Mpita amesema kuwa fedha za vitambulisho ni moja ya mapato ya nchi ambapo amewataka watendaji wa halmashauri kufanya kazi kwa weledi na uaminifu mkubwa .
Hata hivyo, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imegundua uwepo wa akaunti feki iliyokuwa inatumika kuiba fedha za halmashauri, huku Mkurugenzi ambaye uteuzi wake umetenguliwa wiki chache zilizopita, Kazimbaya Makwega Makwega akitajwa kuhusika na akauti hiyo feki iliyokutwa na kiasi cha sh. milioni 83.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list