We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Thursday, May 30, 2019

Ashikiliwa na TAKUKURU kwa kumpa rushwa Mwanasheria wa CCM


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Ilala inawashikilia watu watatu akiwamo mmiliki wa Kampuni ya Motrax, Chandulal Ladwa ambaye anatuhumiwa kutoa rushwa ya Sh 200,000 kwa Wakili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  Goodlucky Mwangomango, ili ampe upendeleo kwenye kikao cha kujadili mikataba ya miradi ya chama hicho. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo, jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Ilala, Christopher Myava amesema, tukio hilo limetokea Mei 29, mwaka huu, saa nne asubuhi, maeneo ya Sea View Upanga kwenye mgahawa wa Central Park. 

Amesema Chandulal ambaye ni mpangaji wa  maeneo ya biashara ya CCM alitoa kiasi hicho ili apewe upendeleo kwenye kikao cha chama hicho cha kufanya marejeo ya mikataba. 

“Mtuhumiwa Chandulal atafikishwa mahakamani chini ya kifungu Cha 15 (1), (b) cha Sheria ya Takukuru Na.11/2007,” amesema Myava. 

Myava alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list