We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, April 29, 2019

Serikali Yaikatalia Kenya kujenga mabwawa ya uzalishaji umeme katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Serikali imeikatalia Kenya kujenga mabwawa ya uzalishaji umeme katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Hayo yamesemwa leo Aprili 29, Bungeni na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantine Kanyasu wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Amina Molel (CCM), ambaye alitaka kujua Tanzania inachukua hatua gani kuhusu suala hilo.

Katika swali lake Amina amesema kuna taarifa kwamba nchi ya Kenya inatarajia kutekeleza mpango wa kujenga mabwawa makubwa kwa ajili ya uzalishaji umeme ambao unatishia ustawi wa uwepo wa hifadhi ya Serengeti.

Akitoa majibu ya swali hilo Kanyasu amesema uchunguzi ulibaini utekelezaji wa miradi hiyo ungesababisha athari kubwa kwa ikolojia ya hifadhi hiyo na utafiti uliofanywa na wataalamu kutoka Kenya kuhalalisha miradi hiyo hazikuwa sahihi.

Aidha Kanyasu amesema miongoni mwa athari hizo ni pamoja na kuhatarisha ustawi na maisha ya viumbe hai kutokana na ukosefu wa maji katika Mto Mara wakati wa Kiangazi.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list