We are currently working on a new website.
Stay tuned for more information.

to stay updated on our progress.

Monday, April 29, 2019

Matawi ya Simba SC kuchangia maandalizi ya Ligi kwa msimu ujao


Na Ahmad Mmow, Lindi

Matawi ya Simba SC mkoani Lindi yamepanga kuchangia maandalizi ya timu hiyo ili iweze kufanya vizuri kwenye  Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL)  na Ligi ya Mabingwa  Barani Afrika (CAFCL) ya msimu ujao.

Hayo yamelezwa wakati wa hafla ya kuipongeza timu ya Simba SC kufikia hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa  Barani Afrika. Hafla ambayo ilifanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Lindi View Resort, iliyopo katika manispaa ya Lindi.

Akizungumza kwaniaba ya matawi ya Mchinga, Nachunyu, Kitomanga na Mitwero ambayo yalituma wawakilishi  kwenye hafla hiyo. Mwenyekiti wa tawi la Mshikamano, Salum Fundi alisema wameamua kuchangia maandalizi ya timu hiyo itakapo kuwa kambini wakati inajiandaa kwa msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania Bara.

Fundi alisema wanajua kwamba Simba ni klabu ya wanachama na licha yakuwa na mwekezaji mwenye asilimia 51 ya hisa, bado wana wanawajibu wa kuchangia ili kumtia nguvu mwekezaji huyo ambaye amesababisha timu hiyo kufikia hatua hiyo kubwa Afrika.


No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Report Abuse

About Me

TAARIFA MPYA KUHUSU APP YETU KAMA BADO HUPATI HABARI ZETU

Habari!! Ni kipindi cha takribani wiki 1 kimepita ukiwa hupati habari, tunaomba radhi kwasababu tumekuwa tukifanya maboresho zaidi. Leo ...

Total Pageviews

Search This Blog

Blog Archive

Labels

Mobile Logo Settings

Mobile Logo Settings
image
recent/hot-posts

Random Posts

3/random/post-list

Recent Posts

3/recent/post-list