RAIS Dkt John Pombe Magufuli amewataka wananchi wa Uyole mkoani Mbeyaamewataka wananchi wa wilaya hiyo kuwa wavumilivu wakati akitafuta njia ya kutatua ombi lao la kupea eneo kwa ajili ya ujuezi wa Kituo cha Mabasi madogo (daladala) na Soko la Uyole.
Magufuli ameyasema hayo leo Jumatatu, Aprili 29, 2019, wakati akizungumza na wananchi hao baada ya Mkuu wa Mkoa huo kumweleza kuwa wanaomba kuchukua sehemu ya neo la Shule ya Msingi Uyole na Sehemu ya Chuo cha Uyole ili kufanikisha ujenzi huo, lakini Rais amesema wampe muda azuzungumze na watalaamu wa ardhi ili waone namna ya kuwapa eneo kwa ajili ya mradi huo.
“Kwani sheria ya ardhi ya mwaka 1996 inaruhusu mgeni kumiliki ardhi? Hilo neo la Wachina lina ukubwa gani? (RC Chalamila akajibu mita za mraba 2,0000). Kwa hiyo ni kama nusu heka. Ndugu zangu nikitoa jibu la haraka nitaharibu, mniachi leo nitazungumza na wataalam wa ardhi, tutalipatia ufumbuzi, najua mmenielewa.
“Watu wa Uyole hawatakiwi kulalamika wakati wananchapa kazi, nimezisikia hizo changamoto naomba mniachie, ‘ahadi ni deni’, hata ulipochomekea la wilaya sijalijibu lakini nimlipokea,” amesema Magufuli.

No comments:
Post a Comment