Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara, Simba leo Ijumaa saa kumi jioni kitashuka kwenye uwanja wa Uhuru kuikabili Mtibwa Sugar katika mchezo wa pili wa ligi kuu ya Vodacom
Simba leo itashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 kwenye mchezo wa kwanza
Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo baada ya mazoezi ya jana yaliyofanyika uwanja wa Uhuru, kocha Patrick Aussems alisema amewaandaa vijana wake kuweza kushinda
Aussems alisema leo Simba itaendelea kumkosa nahodha wake John Bocco aliyeanza mazoezi mepesi hivi karibuni pamoja na Wilker Da Silva ambaye ni majeruhi tangu mwanzoni mwa msimu
Aidha Meddie Kagere alirejea jana kutoka Rwanda alikokuwa na majukumu ya timu ya Taifa, Aussems alisema anaweza kucheza mechi ya leo licha ya kuwa hakufanya mazoezi na wenzie
Kuelekea mchezo huo, takwimu zinaibeba Simba kuweza kufanya vizuri
Msimu uliopita mabingwa hao watetezi walishinda mabao 3-0 mchezo uliopigwa dimba la Uhuru
Kiingilio mzunguuko ni Tsh 5,000/- na VIP ni Tsh 15,000/-

No comments:
Post a Comment